ISIS Kanda Kubwa ya Sahara (ISIS-GS) ilianzishwa mnamo mwaka 2015 baada ya kujitenga kutoka al-Mourabitoun, kundi lililojitenga na al-Qa’ida, na kuapa utii kwa ISIS. Kimsingi likiwa na makao yake nchini Mali na likiendesha shughuli zake kwenye mpaka wa Mali na Nijeri, kundi hili pia lina harakati nchini Bukinafaso. ISIS-GS imedai kuhusika na mashambulio kadha, likiwemo lile la mnamo tarehe 4 mwezi Oktoba, mwaka 2017 dhidi ya doria ya pamoja kati ya Marekani na Nijeri kwenye eneo la Tongo Tongo, nchini Nijeri, ambalo lilisababisha vifo vya wanajeshi wanne wa Marekani na wanne wa Nijeri. Mnamo mwezi Novemba, mwaka 2019, ISIS-GS ilishambulia kambi ya jeshi la Mali na kuwaua wanajeshi 54.
Mnamo tarehe 23 mwezi Mei, mwaka 2018, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marekani ilitaja ISIS-GS kuwa Kundi la Kigaidi la Kigeni chini ya kifungu 219 cha Sheria ya Uhamiaji na Uraia, kama ilivyorekebishwa. Hapo awali, mnamo tarehe 16 mwezi Mei, mwaka 2018, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje iliitaja ISIS-GS kuwa Gaidi wa Kimataifa Mwenye Sifa Maalumu kuambatana na Amri ya Rais 13224, kama ilivyorekebishwa. Matokeo yake ni kwamba, mali yote na maslahi ya ISIS-GS katika mali, vyote vilivyoko chini ya mamlaka ya Marekani vimezuiwa, na watu wa Marekani kwa jumla wamekatazwa kushiriki kwenye miamala yoyote na ISIS-GS. Ni kosa la jinai kutoa kwa makusudi, au kujaribu au kula njama ya kutoa, msaada wa nyenzo au rasilimali kwa ISIS-GS.